Kusimamia Programu ya Huduma kwa Jamii
Thu, 01/21/2016 - 12:24
Jukumu la Idara ya Probesheni na Huduma kwa Jamii ni kusimamia adhabu mbadala katika Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi chini ya Sheria ya Probesheni ya Wahalifu (Kifungu. 247 kilichofanyiwa marekebisho mwaka 2002), Sheria ya Huduma kwa Jamii Na. 6/2002, Kanuni ya Kifungo cha Nje ya mwaka 1968 (EML) na Sheria ya Bodi za Paroli Na. 25/1994.
Sehemu ya Idara hii ni:
- Sehemu ya Probesheni
- Sehemu ya Huduma za Utunduizi
Idara hii inaongozwa na Mkurugenzi akisaidiwa na Wakurugenzi Wasaidizi.