Katika kuendeleza Ushirikiano kati ya Tanzania,Zambia na China ulioanzishwa na Viongozi wa nchi hizo akiwemo Rais wa Awamu ya Kwanza na Baba wa Taifa,Mwalimu Julius Kambarage Nyerere,Kenneth David Kaunda wa Zambia na Rais wa Awamu ya kwanza wa Jamhuri ya Watu wa China,Mao Ze Dong,serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan imeingia makubaliano na China ili kuweza kujenga na kuiboresha Reli ya TAZARA iliyojengwa kutoka mwaka 1970 hadi 1975.