Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Patrobas Katambi, ameahidi kuwa Tume ya Jeshi la Polisi, Magereza, Zimamoto na Uhamiaji itaendelea kufanya maamuzi kwa haki, uadilifu na kwa kuzingatia misingi ya kisheria, akisisitiza kuwa maamuzi yote yatakayofanywa yatatokana na kusikiliza pande zote na kuzingatia sheria na taratibu zilizopo. Waziri Katambi amesema hayo Januari 22, 2026 baada ya uapisho wa kuwa Mwenyekiti wa Tume ya Jeshi la Polisi, Magereza, Zimamoto na Uhamiaji uliofanyika jijini Dodoma ambapo Naibu Waziri,Ayoub Mohamed Mahmoud pia aliapa kuwa Makamu Mwenyekiti wa tume hiyo.