Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
Mkimbizi ni mtu yeyote ambaye kutokana na hofu ya msingi ya
kuteswa kwa sababu za rangi, dini, kabila, uanachama wa kundi la kijamii au
maoni ya kisiasa, yuko nje ya nchi yake au nchi ya maskani yake ya kudumu na
kwamba hawezi au hayuko tayari kuwa chini ya himaya ya Serikali hiyo ambayo
ameikimbia.
Mhamiaji haramu ni raia
wa kigeni aliye ndani ya Tanzania na asiye
na kibali halali cha kuingia au kuishi Tanzania wakati Mkimbizi ni raia wa nchi
ya kigeni aliyeomba na kupewa hifadhi kutokana na kuikimbia nchi yake kwa
sababu za usalama wake
Waomba hifadhi wote wanapowasili nchini wanatakiwa kuripoti katika
Ofisi zozote za Serikali ambako wataelekezwa kufika Idara ya Wakimbizi au
kuonana na “Ofisa aliyeidhinishwa” ambaye
atawapa utaratibu wa kufuata kufika Ofisi za Idara ambako watahojiwa na kusajiliwa.
Ifahamike kwamba maeneo wanayoishi wakimbizi ni maeneo tengefu, hivyo
wageni wote wanaotaka kuingia katika maeneo haya kwa ajili ya kutoa huduma au
sababu zozote zile; watapaswa kuandika barua ya kuomba kibali kwa Mkurugenzi wa
Idara ya Huduma kwa Wakimbizi. Hairuhusiwi kuingia maeneo tengefu bila kibali.
Usafirishaji haramu wa binadamu unahusisha kitendo cha
kuajiri, kusafirisha, kuficha au kupokea mtu kwa njia ya vitisho, nguvu,
udanganyifu au matumizi mabaya ya madaraka kwa lengo la unyonyaji. Unyonyaji
unaweza kuwa wa kazi za kulazimishwa, ukahaba, kufanya kazi za ndani, kulazimishwa
kuomba mtaani au kushirikishwa katika vitendo vya uhalifu.
Viini vinavyounda kosa la usafirishaji haramu wa binadamu
ni;
· Tendo
Lenyewe: Kusajili, Kusafirisha, kuhamisha, kuhifadhi, kutoa au
kupokea mtu kwa ajili ya kumtumikisha
· Mbinu:
kudanganya, kutisha au kutumia nguvu, kuteka na kutumia mikataba ya uongo
· Nia/Kusudio:
kutumikisha kingono, kufanyisha kazi ngumu, kulazimisha kuomba mitaani, kutoa
viungo vya mwili na kufanyisha kazi za ndani
Ndiyo. Usafirishaji haramu wa binadamu ni kosa la jinai
chini ya Sheria ya Kuzuia Usafirishaji Haramu wa Binadamu, Sura ya 432.
Wahalifu hukabiliwa na adhabu kali ikiwemo kifungo cha maisha Gerezani.
Dalili ni pamoja na: haruhusiwi kuondoka sehemu ya kazi, kunyanganywa nyaraka binafsi, kufanya kazi kwa muda mrefu bila malipo au kwa malipo kidogo, anakula mabaki ya chakula kilichoachwa na mwajiri wake, ana makovu au vidonda ambavyo havijatibiwa kutokana na kuteswa, kuonyesha hofu au wasiwasi uliopitiliza, na kutumikishwa kwenye ukahaba au kazi za kinyonyaji.
Mtu yeyote anaweza kusafirishwa kiharamu, lakini makundi
yaliyo hatarini zaidi ni wanawake, watoto, watu wenye ulemavu, maskini na
wahamiaji wanaotafuta fursa.
Vichocheo ni pamoja na umaskini, ukosefu wa ajira, mahitaji
ya nguvu kazi ya bei nafuu, ukahaba, migogoro ya kifamilia, ukosefu wa elimu, utandawazi,
tamaa ya maisha mazuri na faida kubwa wanayoipata wahalifu wanaojihusisha na
biashara hii.
Magendo kwa wahamaji yanahusisha kuvuka mipaka kinyume cha
sheria kwa ridhaa ya mhusika, na mara nyingi huishia baada ya kuwasili eneo
analokwenda. Usafirishaji haramu wa binadamu unahusisha unyonyaji, mara nyingi
bila ridhaa, na huendelea hata baada ya kufika mwisho wa safari.
Kwa Waathirika: mateso, msongo wa mawazo, unyanyapaa,
magonjwa, kupoteza uhuru na kifo. Kwa Familia: utengano, mzigo wa kifedha. Kwa
Taifa: hasara ya kiuchumi, machafuko ya kijamii na kudhalilika kimataifa.
Kupitia Sheria ya Kuzuia Usafirishaji Haramu wa Binadamu
(Sura 432), kupitia Sekretarieti ya Kuzuia na Kupambana na Usafirshaji Haramu
wa Binadamu, kampeni za uelimishaji, mafunzo na ushirikiano na taasisi mbalimbali
zikiwemo za kimataifa.
Ripoti mara moja katika kituo cha Polisi, piga simu kwenye
namba ya dharura 195 ya Sekretarieti ya Kuzuia Usafirishaji Haramu wa Binadamu,
au toa taarifa kwa viongozi wa eneo husika.
Waathirika hupata msaada wa uokoaji, makazi salama ya muda,
huduma za afya, ushauri, msaada wa kisheria, utafutaji wa familia, msaada wa
kurejeshwa kwenye jamii, na ulinzi wa haki na utambulisho wao.
Kujielimisha, kuripoti matukio yanayotiliwa shaka, kusaidia
familia zilizo hatarini, na kuelimisha jamii kupitia shule, makanisa, misikiti
na mikutano ya kijamii.
Tembelea ofisi ya Sekretarieti au tovuti ya Wizara ya Mambo
ya Ndani ya Nchi, fuatilia kampeni za uelimishaji, au piga simu kwa namba ya
dharura 195.